MwanzoUSD / KES • Sarafu
add
USD / KES
Bei iliyotangulia
128.48
Habari za soko
Kuhusu Dola ya Marekani
Dolar ya Marekani ni pesa halali ya Marekani. Alama yake ni $.
Dolar ya Marekani inapatikana kwa noti za dola 1, 2, 5, 10, 20, 50 na 100. Kuna pia sarafu ya dola 1.
Dolar moja ina senti 100. Senti huitwa pia "penny" nchini Marekani. Kuna sarafu za nusu dolar, robo dolar na sarafu za senti 10, 5 na 1.
Hadi mwaka 1969 noti ya dolar ya Marekani ilikuwa na ahadi ya kwamba serikali ya Marekani itampatia kila mtu dhahabu kulingana na thamani ya dola hizi akipenda kuzibadilisha.
Usawa huu na thamani ya dhahabu ulifutwa. Leo hii dolar ya Marekani ni pesa ya kuiamini serikali kama pesa zote. Maana yake watumiaji husadiki ya kwamba serikali haitachapisha dola kushinda uwezo wa uchumi na thamani ya bidhaa zilizopo nchini Tanzania.
Tangu mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia dolar ya Marekani imekuwa pesa kuu duniani na sehemu kubwa ya biashara ya kimataifa hukadiriwa kwa dolar hizo. Lakini tangu kupatikana kwa Euro mwaka 1999 umuhimu wa dolar ya Marekani imeanza kupungua polepole. Hata hivyo nchi mbalimbali zimeachana na sarafu zao na kuamua kutumia dolar ya Marekani tu, k.mf. El Salvador. WikipediaKuhusu Shilingi ya Kenya
Shilingi ya Kenya ni fedha za Kenya. Shilingi moja imegawanywa kwenye senti mia moja.
Shilingi ya Kenya ilianzishwa mwaka 1966 baada ya kuvunjwa kwa bodi ya fedha ya Afrika ya Mashariki iliyosimamia fedha ya pamoja ya Kenya, Tanzania na Uganda iliyoitwa East African Shilling iliyotumiwa katika maeneo yote yaliyokuwa chini ya Uingereza katika Afrika ya Mashariki.
Kuna sarafu za shilingi 1, 5, 10, 20 na 40.
Sarafu za senti zipo za zamani za senti 1, 5, 10, 20 na 50 lakini hazinunui kitu tena.
Noti zilitolewa za shilingi 5, 10, 20, 50, 100, 200, 500 na 1000 ingawaje noti za shilingi 5, 10 na 20 ni nadra sana kuonekana.
Shilingi 1 = Senti 100
Majina ya zamani:
Thumuni 1 = Senti 50
Peni 1 = Senti 10
Ndururu 1 = Senti 5 Wikipedia